Showing posts with label Biashara. Show all posts
Showing posts with label Biashara. Show all posts

Sunday, April 7, 2019

Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX nchini yatoa offer mpya kwa wale wanaotaka kutangaza biashara zao kimataifa

adpollex
Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX iliyojikita Afrika Mashariki kwenye shughuli za utangazaji sasa imezindua offer mpya ya kukupa nafasi mteja wetu kutangaza biashara/kampuni yako kimataifa kwa sasa kampuni imeaonyesha nia ya dhati ya kuwekeza kwa wajasiriamali wadogowadogo hili kuwazesha wafanyabiashara wadogo kuwekeza kwenye matangazo ili kuongeza mapato yao. Uwekezaji huu unatarajiwa kuongeza tija na muamko wa wafanyakazi na wateja wao. Kufuatia mabadiliko haya sasa kampuni ya ADPOLLEX  itaweza kuhudumia wateja wake kwa viwango vya juu zaidi huku idadi ya wabunifu na vitendea kazi vikiongezwa.
Akizindua OFFER hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam mwekezaji huyo Bwana CHRISPER MALAMSHA amesema, “nia na madhumini ya uzinduzi huu ni kuitambulisha kampuni hii kwa upya kwa watanzania, licha ya kuwapo hapa nchini kwa zaidi ya miaka miwili.
MALAMSHA aliendelea kusema “soko la Tanzania kwa sasa linakua kwa kasi na sekta ya ushirikiano inazidi kukua kwa viwango vya juu, hivyo umuhimu wa kutangaza masoko na bidhaa zinazozalishwa ni mkubwa mno, kwa kufanya hivi tunatoa nafasi kwa makampuni mengine kutambua uwepo wetu hapa Tanzania na Afrika mashariki na wao kuweza kuzitambua kazi tunazozifanya.
”Kufuatia uwekezaji huu mpya na kukutangazia kampuni yako kimataifa, nia kubwa ni kukuza sekta ya masoko kwa Afrika mashariki huku tukifanya kazi kwenye viwango vya kimataifa. Tunayofuraha kubwa kwa uwekezaji huu kwani utaongeza tija kwa watanzania wenye vipaji.
Kampuni ya ADPOLLEX inatoa huduma mbalimbali kama kuandaa matangazo ya biashara kwa niaba ya wateja, kununua nafasi za matangazo kwenye vyombo vya habari, kuandaa mikakati ya jinsi ya kukuza bidhaa yako, kuwatangazia wateja bidhaa zao kwenye mitandao mbalimbali na kuwashauri hali halisi ya masoko na ushindani ilivyo duniani kwa sasa.
“Ni furaha kubwa kuitambulisha kwenu kampuni ya ADPOLLEX” alisema Bw Daniel Octavian, Meneja Mkuu wa ADPOLLEX Tanzania, huku tukijivunia timu yenye wafanyakazi bora na kazi nzuri ambazo tumeshazifanya mpaka sasa kwa wateja wetu,licha ya kuandaa kazi nzuri zilizoendana na soko la wateja wetu lakini pia tumeonekana kimataifa na kupata nafasi ya kushiriki kwenye baadhi ya forum mbalimbali duniani kwenye sekta ya matangazo. Ushiriki huu utakuwa na manufaa makubwa kwa wateja wetu na kutuwezesha sisi kama ADPOLLEX kupanua wigo wetu wa kufanya kazi kimataifa.
Dhamira yetu ni kuona ushindani wa matangazo ya bidhaa kwa Tanzania unakua na kufikia viwango vya kimataifa.
Bw Daniel aliendeela kusema “Kama kampuni tumefanya kazi hapa Tanzania kwa miaka miwili na makampuni ya ndani na nje ya Tanzania ikiwamo makampuni ya simu, benki, taasisi zisizo za kiserikali,kampuni za samani za ndani, kampuni za sola na nyingine nyingi. Kwa miaka hiyo michache ya kufanya kazi kwa bidii na kutambulika kimataifa,kampuni ya ADPOLLEX sasa inasababu ya kujivunia ujuzi wa kufanya kazi za wazawa huku tukizifanya kwa viwango vya kimataifa. Kama wadau wa matangazo tunaamini ubunifu bora unaleta ushindani katika soko na kuweza kuifikisha bidhaa kwenye viwango vya kimataifa.
GudyTV

Saturday, April 22, 2017

Njia Tano (5) Bora Za Kupata Mtaji Wa Kuanza Au Kukuza Biashara


Moja ya changamoto ambazo watu wengi wanaotutafuta huwa ni wanawezaje kupata mtaji wa kuanza biashara. Hiki kimekuwa kikwazo kwa watu wengi kuingia kwenye biashara. Hata wale ambao tayari wapo kwenye biashara, wamekuwa wakitamani kukuza biashara zao ila wanashindwa kutokana na kukosa fedha za kuingiza kwenye biashara.

Tatizo kubwa ambalo linawazuia wengi kutopata mtaji wa biashara ni kwa sababu inapokuja swala la mtaji wanafikiria sehemu moja tu, ambayo ni mkopo. Na kwa bahati mbaya sana watu wengi wanakuwa hawana sifa zinazowawezesha kupata mkopo wa kibiashara. Kwa kukosa sifa hizo huishia kukaa na kulalamika nataka kuingia kwenye biashara ila mtaji sina.

Kama wewe unapenda biashara, na umepanga kuingia au umeshaingia lakini hujaweza kukuza mtaji wako, hapa tutakupa njia mbalimbali za kupata mkopo kwa ajili ya biashara yako.


  1. Fedha zako binafsi.
Njia nzuri sana kwako kupata mtaji wa biashara ni kwa kuanza kuweka akiba ya fedha zako mwenyewe. Kama umeajiriwa anza utaratibu maalumu wa kuweka kiasi cha fedha pembeni ambacho hutakigusa hata iweje. Baadae unaweza kukitumia kwenye kuanza biashara. Kama hujaajiriwa unaweza kutafuta shughuli yoyote ukafanya na hii ikakuingizia kipato ambacho baadae utaweza kuanzia biashara.


  1. Michango kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki.
Kama unaweza kukaa chini na ndugu zako na ukawashawishi vizuri, watakuwa tayari kukuchangia uanze biashara. Kama watu wanaweza kuchangia harusi na mambo mengine, wanaweza pia kuchangia biashara, ni wewe uweze kuwashawishi vizuri. Ila hapa unahitaji kuwa unaaminika na ndugu hao n apia waoneshe ni jinsi gani wao watanufaika na biashara utakayoanzisha.


  1. Kutafuta mtu au watu wa kushirikiana nao.
Kwa uzoefu wetu, kuna watu wengi ambao wana mitaji ya kibiashara ila hawajui ni biashara gani wafanye au hawana muda wa kusimamia biashara. Na wakianzisha biashara kwa sababu hawana usimamizi mzuri wanapata hasara. Sasa wewe unahitaji kuwajua watu wa aina hii na andaa mpango ambao utawashirikisha na kuonesha ni kwa jinsi gani mkiungana pamoja mnaweza kuwa na biashara nzuri na yenye faida. Hii pia inahitaji uwe unaaminika na yule unayempelekea mpango wako.


  1. Kuanza biashara kwa fedha za mteja.
Hapa unaweza kukusanya fedha kwa wateja kwanza halafu ndio ukawapata huduma au bidhaa wanayohitaji. Kama utaweza kuwa na mpango mzuri wa biashara ambapo mteja anahitaji sana unachotoa, na tayari anakuamini anaweza kukupa sehemu ya gharama na wewe kutumia gharama hiyo kumpatia bidhaa au huduma anayotaka. Hii pia inahitaji uaminifu na wale unaofanya nao biashara.

Hii ndio njia ambayo inafahamika na kila mtu na watu ndio huwa wanaifikiria hii kila wanapofikiria mkopo wa biashara. Kama una sifa za kupata mkopo unaweza kuchukua mkopo na kuutumia kwenye biashara. Ila kuwa makini sana kama unachukua mkopo kwa ajili ya kuanzia biashara, ni hatari sana na unaweza kujiingiza kwenye matatizo zaidi.

Bado unafikiria ni njia gani unazoweza kutumia kupata mkopo wa biashara? Anza na hizo hapo juu na boresha kadiri biashara yako ilivyo na wale wanaokuzunguka walivyo. Hakuna kitu kinachoshindikana kama utaamua kweli kupata mkopo wa biashara.
 

Sunday, April 2, 2017

MAKOSA MATATU YANAYOZUIA USIPATE WATEJA UNAPOTANGAZA BIASHARA



Kama ungependa kupata wateja na kuongeza mauzo katika kampuni au biashara yako, lazima utambue na kuyaepuka makosa yanayofanya usiuze unapotangaza biashara yako. Wateja na mauzo ndio uhai wa biashara yako.
Makosa nilio ainisha hapa, nina uhakika yanazuia mfanyabiashara asipate wateja pindi anapotangaza. Katika kipindi cha mwanzo mwaka 2015 wakati naanza kufanya biashara na kutafuta Business partners, mauzo yangu na hata kupata Business partners haikuwa kazi rahisi, hadi  nilipogundua haya makosa niliokuwa nikiyafanya na kujifunza jinsi ya kuyaepuka.

 WATU HAWASOMI MATANGAZO YAKO. 

Matangazo ndiyo huanza kuitambulisha biashara kwa wateja wako. Ikiwa utafungua biashara kisha ukatulia au unatangaza lakini watu hawasomi matangazo yako, hakuna atakayejua unatoa huduma au bidhaa au ofa. Kibaya cha jitangaza kizuri cha jiuza, kauli hii ipe kisogo kama biashara ndio inaanza lazima ujue jinsi ya kuitangaza.
Kwa nini watu hawasomi tangazo lako? 

• Headline(kichwa cha tangazo) 

Kama umeweka tangazo  katika Mitandao ya kijamii, barua pepe au umebandika mahali watu wanaliona lakin wanalipita bila kulisoma, hapo tatizo la kwanza lipo kwenye headline (kichwa cha tangazo).
Headline ndio inamfanya msomaji amue ndani ya muda wa sekunde 3 hadi 10 kusimama asome tangazo lako au apitilize. Kwenye Internet wasomaji wanafanya maamuzi haraka sana ndani ya sekunde 3, atakuwa ameamua kusoma makala au tangazo lako au abonyeze kitufe aendelee na safari kulingana na Headline.
Tengeneza vichwa hata zaidi ya vitano vya tangazo lako kisha uchague. Headline ya kwanza kujitokeza kichwani, inaweza isiwe nzuri kuliko utakazo zipata ukiendelea kufikiria.

• Mwanzo wa Tangazo 

Sentensi ya mwanzo baada ya tangazo. Ni muhimu kuwa na mvuto wa kumfanya msomaji atake kuendelea kusoma yaliyomo ndani ya tangazo.
Mfano:
Kama ungependa kupata wateja na mauzo…..
Kama ungependa kupata bidhaa bora na zenyekutatua…..
Sasa unaweza kupata/kupokea/kutumia….
Mifano miwili hapo nimetoa kukupa mwanga, ujifunze jinsi ya kumlazimisha msomaji aendelee kusoma yanayofuata katika tangazo lako.

2. HULENGI WATEJA HUSIKA (BAD TRAGERTING)

Watu watasoma tangazo lako, lakini hutaweza kuwabadili kuwa wateja kama tangazo umeandika vizuri lakini hukufanya utafiti mzuri ni wapi utapata wateja wako.  Unajikuta umepeleka tangazo au bidhaa kwa wasio wahitaji. Ni kana vile umekwenda kutangaza au kuuza Computer kwa ambao hawahitaji na hawaju au kuuza nguruwe msikitini.
Jinsi ya kufanya target ya wateja:

Kabla ya kuanza biashara fanya tafiti kuhusu wateja, unatakiwa kufahamu wateja wako ni akina nani na sifa zao ni zipi. Sifa za kutambua kwa wateja:

Jinsia: Mke/Me
Umri:  18 – 45 (mfano)
Kipato: ********
Elimu: ********

Baada ya kutambua wateja wako, fanya jitihada za kufahamu  wapi utawapata.

Wateja wako wanapatikana sehemu mbalimbali kutegemeana na sifa za wateja wako. Mfano wanaweza patikana:
Magrupu ya ujasiriamali katika mitandao ya kijamii.
Sehemu za michezo
Mashuleni
Katika forum mbalimbali ujasiriamali, michezo, mapenzi, siasa n.k(itategemeana na wewe biashara)
Usipokuwa tambua wateja wako vizuri na kufahamu wapi wanapatikana ndio unajikuta, unapoteza muda kutangaza bidhaa au huduma kwa watu ambao hawatumii biashara yako.
Watu wananunua au kulipia vitu ambavyo wanafikri vitatua matatizo walio nayo. Wananunua vitu wanavyohitaji wanaacha ambavyo hawahitaji. Hivyo ili uuze lazima ufanye target ya wateja, ukitaka kila mtu umuuzie utatumia muda na pesa yako lakini matokeo yanakuwa hafifu.

Hatua ya tatu ni kuweka mikakati ya kufika mahali wateja wako walipo.

Katika hatua hii ndio unaandaa matangazo kwa kuzingatia sifa za wateja wako kisha unapeleka tangazo mahali walipo.

3.  HUTOI OFA KWA WATEJA

Ofa inamfanya mteja ambaye hajawahi kuitumia bidhaa au huduma yako kupata nafasi ya kuijaribu huduma au biashara yako. Mteja anakuwa na mashaka na ubora wa bidhaa yako na wewe mwenyewe muuzaji.
Nini cha kufanya kumwondoa hofu mteja?

Kama mteja ana hofu na wewe, jitihadi kuwa unajifunza mbinu, maswali na jinsi ya kumsaidia mteja kufikia maamuzi ya kufanya manunuzi.
Unapotangaza biashara yako kumbuka kuweka ofa, chagua ofa ambayo haikuathiri, ofa zipo nyingi sio lazima utoe bidhaa zako bure 100%, unaweza:
Kuanza kutoa thamani ya huduma yako, wateja wako wakikuamini basi wanakujoin.
Toa punguzo katika kipindi maalumu, baada ya muda husika wa ofa, rudisha bei kama ilivyokuwa.
Ukitoa ofa ya punguzo toa tangazo. Kumbuka kuweka muda wa mwisho wa ofa. Muda wa mwisho unapokaribia mteja akiona tangazo huwa anahamasika kufanya maamuzi ikiwa tangazo linamhusu.


4. BIDHAA/HUDUMA YAKO HAIKIDHI HITAJI LA MTEJA

Je, mteja wako anapata alichotarajia kupata wakati akinunua huduma yako?? Kama umelenga vema wateja husika, lakini bidhaa hazina ubora au hazitatui hutaji husika la mteja, kuna uwezekano wa kupoteza wateja. Mteja hataweza kurudi kununua bidhaa yako kama alinunua akakutana na hali ambayo haikumridhisha.
Fanya jitihada tangu unapoanza biashara, chagua biashara ambayo itagusa wengi, kama ni huduma toa huduma anbayo itagusa wengi.
Kwa makala nyingine kuhusu masoko na mbinu za kupata wateja kupitia mitandao ya kijamii, tembelea page yangu: Shori MN(page)  au blog: shori success life

 

Wednesday, August 10, 2016

TANGAZA BIASHARA YAKO NA BAN MARKETZ UPATE WATEJA WENGI ZAIDI


  Ban Marketz inakupa fursa wewe Mfanya Biashara Kuweza kutangaza Biashara yako kwa Bei nafuu na kwa urahisi zaidi.
Tangaza Biashara yako nasi ili uweze kufikia malengo uliyo jiwekea katika Biashara yako, Ban Marketz inauwezo mkubwa wa kutangaza Biashara yoyote ile kama vile Maduka, Bidhaa, Mikutano, Viwanja na Mashamba, Nyumba na Partment. Pia tunapokea matangazo yoyoye isipo kuwa matangazo yasioruhusiwa na serikali yaani kisheria..

Mahitaji yetu ni Picha za Product yako unazo taka kutangaza (zisizidi picha 10 ) na maelezo ya Product yako pamoja na Contact zako na Location Ulipo..

Ban Marketz  ina miliki pages,groups tofauti kwenye social media zote zinazotembelewa kwa sasa inapata PAGE VIEWS (yani Kusomwa mara ) laki 6 mpaka 1,000,000 kwa Siku moja na kwa Mwezi Ban Marketz inapata PAGE VIEWS (Kusomwa mara )Milion 12,500,000 kwa uwezo huu tulionao Ban Marketz itaweza kuitangaza Bishara yako na kuweza kuwafikia watu wengi zaidi ndani na nje ya nchi..
Kwa mawasiliano nasi 0684320325, 0768 320325, 0656704111 Namba zote zinapatikana.

Tuesday, June 28, 2016

Njia 5 zinazoweza kukufanya Msanii huonekane International kwa gharama nafuu



Njia 5 zinazoweza kukufanya Msanii huonekane International kwa gharama nafuu

1.  Kufanya kazi kwa bidii
        Usikae muda mrefu bila kuachia nyimbo ili kuwafanya watu wako wasikusahau aau washawishike
        kuhamia/kutafuta radha kwa wasanii wengine.

2.  Kukubali kukosolewa
        Ukikubali kukosolewa na kuifanya kuwa changamoto katika kazi zako zijazo kwa njia ya mabadiliko 
        kama mashabiki wako wanavyopenda huwe.

3.   Heshima
       Kumheshimu kila mtu hasa mashabiki zako kwa maana ukimdharau mteja wako na akagundua
       unamdharau hawezi kuwa mshabiki wako tena kwani hajivunii uwepo wako kama hautomheshimu kwa
       namna moja au nyingine.

4.   Mabadiliko
      Mabadiliko kwa msanii ni lazima chamsingi asitoke nje ya misingi aliyojiwekea ili atambulike anafanya
      kitu gani au mziki wa aina gani,

5.  Kuwa karibu na mashabiki zako
     Ili kufanikisha hili la kuwa karibu na mashabiki zako, inamaana uwe karibu na media (mitandao ya
     kijamii)  kama vile facebook,twitter,instagram, na mingine, kushiriki mambo ya kijamii kwa michango ya
     hali na mali .Ikibidi tafuta kampuni ambayo inaweza kukufanyia mipangilio mizuri katika pages zako ili wakufanyie promotion ya kazi zako. mf. BanMarketz

Wednesday, June 8, 2016

Jifunze namna ya kuanzisha biashara yako kwa njia sahihi

Jifunze namna ya kuanzisha biashara Kwenye thread hii nimeona wengi wamepost hoja ya kutaka ushauri wa kuanzisha biashara, na wengine wameenda mbali zaidi kwa kutaja kiwango cha pesa alicho nacho kwamba ni biashara gani itafaa. Lakini inaonyosha dalili kwamba waanzaji wengi wa biashara wanakimbilia kuanzisha biashara kabla ya kupanga mikakati ya utafiti kwa kutumia kigezo cha business plan. Ni dhahiri uanzishwaji wa biashara ambayo itasajiliwa serikalini na kulipia kodi ni tofauti na mfumo wa biashara za kimachinga ambao hununua na kuuza eneo analotaka na sipopata wateja huhamia eneo jingine.

Business Plan ni jambo la kwanza na la msingi katika uanzishwaji wa biashara yako. Mambo ya msingi unayotakiwa kufanya katika business plan yako ni kama ifuatavyo:

  • Aina ya biashara unayokusudia kuanza
  • Wateja walengwa kwa biashara yako wanaoishi maeneo hayo, wanaopita maeneo hayo nk.
  • Eneo la kufanyia biashara yako ukitilia maanani kuchunguza ushindani wa biashara uliopo katika eneo hilo.
  • Fanya utafiti na wafanyabiashra wengine ambao wana uzoefu na biashara hiyo ili kupata mwelekeo wa biashara yako.
  • Fanya utafiti wa source ya kupata bidhaa kutoka makampuni yanayouza na tafiti ni kampuni ipi yenye maslahi kwako.
  • Andaa mfumo wa gharama za uendeshaji wa biashara ikiwa ni pamoja na Mtaji wako,
  • Gharama za uendeshaji ikiwa ni pamoja na gharama za uanzaji wa bishara, vitendea kazi, kulipia pango, tax, umeme, usafiri, simu, mishahara, nk. (Kumbuka wewe unalipwa mshahara pia na umeajiriwa na biashara yako).
  • Kisha tathmini faida utakayopata baada ya gharama za uendeshaji na kumbuka biashara inasimama ambayo ina net profit, gross profit tu ni hasara.
Mtaji ulio nao usiuhesabu kama ndio kianzio cha biashara yako, maana kuna gharama za maandalizi ya mahali utakapoweka biashara yako, leseni za biashara pamoja na vitendea kazi vingine. Hivyo vyote uvifanyie mahesabu katika gharama za uanzishwaji wa biashara yako.
Hakikisha theluthi moja ya mtaji wako wa pesa umebaki kwa ajili ya uendeshaji wa biashara yako maana biashara hadi isimame na kuanza kujiendesha yenyewe huchukua wastani wa miezi 6 kama upo eneo lenye wateja wazuri.

Huu ni ushauri wangu binafsi, nategemea kuna wengi hapa wenye ushauri mzuri zaidi watajazia yaliyopungua.